Michael van Gerwen atinga nane bora

♠ Posted by Unknown at 23:07

Michael Van Gerwen

Mchezaji wa mchezo wa Vishale Michael van Gerwen,amefanikiwa kuingia hatua ya nane bora katika michezo ya dunia kwa kumfunga Terry Jenkins kwa mabao 4-1

Katika michezo mingine Robert Thornton pia aliibuka kidedea kwa kumchapa Benito van de Pas kwa mabao 4-0 na atachuana na Van Gerwen katika hatua ya robo fainali.
Raymond van Barneveld alifanikiwa kuingia robo kwa kupata ushindi wa 4-3 dhidi ya mpinzani wake Jamie Caven.
Huku Stephen Bunting akishinda kwa ushindi wa 4-1 mbele ya James Wade, Mwingereza Smith alipata ushindi licha ya kutanguliwa kwa 2-0 kwenye awamu ya kwanza na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa 4-2 dhidi ya Brendan Dolan.
Mchezaji wa Uholanzi Vincent van der Voort alimaliza kwa kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 kwa kumtwanga Max Hopp toka Ujerumani.

0 comments:

Chapisha Maoni