STEVE RNB ATANGAZA NDOA, BARNABA AMTOLEA MAHARI MAMA STEVE

♠ Posted by Unknown at 22:08

MSANII wa Bongo Fleva, Steven William ‘RnB’ juzikati aliweka wazi kuwa anatarajia kuoa Oktoba 11, mwaka huu huku mwanamuziki mwenzake Elias Barnaba akieleza kuwa amemtolea mahari mzazi mwenzake, mama Steve na siku si nyingi atafunga ndoa.
Msanii wa Bongo Fleva, Elias Barnaba.
Wakizungumza na Ijumaa kwa nyakati tofauti, wasanii hao kila mmoja ameonesha dhamira ya kuishi katika njia inayompendeza Mungu.“Nimeamua kuachana na maisha ya ukapera hivyo mwezi ujao natarajia kuhalalisha maisha ya ndoa na mchumba wangu Ester Emmanuel,” alisema Steve.
Msanii wa Bongo Fleva, Steven William ‘RnB’.

Naye Barnaba alisema: “Nimegundua hakuna mwanamke mwingine atakayenifaa zaidi ya mama Steve, nasema hivi kulingana na historia yetu tangu tunakutana hadi leo, kanivumilia sana na sasa ni vyema nikamfanya awe mke wangu halali.”

0 comments:

Chapisha Maoni