MWILI WA JAJI MAKAME WAAGWA NA KUSAFIRISHWA LEO

♠ Posted by Unknown at 08:07


 
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akisaini kitabu cha maombolezo.

 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulahman Kinana akisaini kitabu cha maombolezo.
 
Familia ya Jaji Makame wakiwa na huzuni.
 
Jaji Mkuu Mohamed Othman Chande akitoa pole kwa mwanafamilia, nyuma yake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar, Said Mecky Sadick.
 
Jaji mstaafu Joseph Sinde Warioba akitoa pole kwa familia ya Makame.
 
Rais wa awamu ya pili, Ally Hassani Mwinyi akitoa pole kwa familia ya Makame.
 
Waziri Mkuu akitoa pole kwa wafiwa kwa niaba ya Watanzania.
 
Kushoto ni Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumayi, Joseph Warioba, Jaji Mkuu Mohamed Athuman Chande pamoja Na Waziri Mkuu Pinda wakiwa msibani.
 
Viongozi mbalimbali na wanafamilia wakiaga mwili wa marehemu  jaji Makame.
 
Jeneza la  marehemu Jaji Makame likibebwa tayari kuingizwa kwenye gari.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewaongoza Watanzania kuuaga mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu  Lewis Makame ambao umeagwa  leo katika Viwanja vya Karimjee na kisha kupelekwa katika  Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano Upanga kwa maombi na kisha kusafirishwa kuelekea Muheza mkoani Tanga kwa ajili ya mazishi.

0 comments:

Chapisha Maoni